Test Footer

Michezo

                                            Haruna Moshi kurejeshwa Taifa Stars

Kwani Poulsen aliweza kuwaita washambuliaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu, wanaoichezea Klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Mbali na hilo Kiungo Mshambuliaji wa Simba Haruna Moshi 'Boban', ni miongoni mwa majina 25 ya kikosi yaliyoanikwa na Kocha wa Timu ya Soka ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars', Kim Poulsen kinachojiandaa kwa mchezo wa kufuzu kwa fainali z Mataifa ya Afrika dhidi ya Ivory Coast.
Kocha huyo aliweza kumtema Nahodha wa timu hiyo Shadrack Nsajigwa wakiwemo na viungo wengine Nadir Haroub ‘Canavaro’ wote kutoka Yanga, Henry Joseph wa Kongsivinger ya Norway, Danny Mrwanda wa DT Long
An ya Vietnam na kiungo aliyefungashiwa virago na timu ya Philadephia Nizar Khalfan.
Alisema kikosi hicho kitaingia kambini kesho hapa Jijini, na uteuzi wake uwezingatia uwezo wa mchezaji kwa nafasi anayochezea na uwiano kwenye nafasi zote ndani ya kikosi cha timu hiyo.
Akitetea uamuzi wake wa kumrudisha kwenye kikosi cha timu hiyo kiungo mwenye rekodi ya utovu wa nidhamu Boban, alisema kuwa anampa nafasi nyingine mchezaji huyo kwani ameonesha uwezo mkubwa kwenye timu yake ya Simba msimu huu.
Mbali na kiungo huyo kurejeshwa pia alimrejesha mfungaji bora wa Ligi Kuu John Bocco wa Azam, aliyetangaza kustaafu soka la Kimataifa kutokana na kuzomewa mara kwa mara na mashabiki kila anapoichezea timu ya taifa.
Alisema kuwa amemuita mshambuliaji huyo baada ya kuzungumza naye na kufanikiwa kumshawishi kubadili uamuzi wake.
Amemuacha Nahodha Nsajigwa kutokana na kuwa kwenye kiwango cha chini kwa sasa na timu yake ya Yanga, kuwa kwenye msimu mbaya, sababu ambayo pia ameielezea kwa Canavarro.
Kuhusu kuacha wachezaji wanaocheza nje ya nchi alisema wachezaji hao wana viwango sawa na wachezaji wanaocheza soka hapa nyumbani na kwamba wanatakiwa kuwa na viwango vya juu kuliko vya nyota wanaocheza ndani.
Kim pia amewajumuisha kwenye kikosi chake wachezaji kadhaa wa timu ya Taifa ya Vijana na chipukizi toka Simba, ambao ni Simon Msuva (Moro United- U20), Frank Domayo (JKT Ruvu- U 20), Edward Christopher (Simba), Jonas Mkude (Simba-U 20) na Ramadhani Singano (Simba-U 20).
Kikosi kamili cha timu hiyo kinaundwa na makipa: Juma Kaseja (Simba), Mwadini Ally (Azam) na Deogratius Munishi (Mtibwa Sugar).
Mabeki ni Nassor Masoud ‘Cholo’ (Simba), Aggrey Morris (Azam), Amir Maftah (Simba), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Simba), Waziri Salum (Azam), Shomari Kapombe (Simba) na Juma Nyoso (Simba).
Viungo ni Mwinyi Kazimoto (Simba), Salum Abubakar (Azam), Nurdin Bakari (Yanga), Jonas Mkude (Simba), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Edward Christopher (Simba- U20), Mrisho Ngasa (Azam) na Frank Domayo (JKT Ruvu- U20).
Washambuliaji ni Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Ramadhan Singano (Simba-U20), Simon Msuva (Moro United- U20), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Haruna Moshi ‘Boban’ (Simba) na John Bocco (Azam).
Stars inayodhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Kilimanjaro itacheza mechi ya kirafiki nyumbani Mei 26 dhidi ya Malawi kabla ya kuivaa Ivory Coast ugenini Juni 2 jijini Abidjan.

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. KILWA FORUMS - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website
Proudly powered by Blogger