Test Footer

Home » » UDOM sasa kufundisha kwa MTANDAO!

UDOM sasa kufundisha kwa MTANDAO!

Written By mahamoud on Tuesday, May 15, 2012 | 1:21 PM

Katika kuhakikisha kuwa tunakwenda na kasi ya teknologia inayoenda kwa kasi duniani, Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) sasa kimeanza rasmi kufundisha kwa kutumia mtandao na kuhakikisha
kila mhadhiri, anafundisha madenti wengi kwa wakati mmoja.
Hilo liliwekwa wazi juzi na Balozi Juma Mwapachu, alipokuwa akizungumza na wahadhiri wa Udom katika ufunguzi wa mafunzo ya ufundishaji kwa njia ya teknolojia hiyo.
Mwapacha ambaye pia ni Mwenyekiti wa baraza la chuo hicho, alisema wingi wa wanafunzi katika chuo hicho kikubwa kwa sasa hauendani na idadi ya wahadhiri waliopo na kwamba bila ya  kuwa na mbinu mbadala za kuwafundisha, wanafunzi wataachwa nyuma.
 “Udom sio chuo cha kawaida katika nchi za Afrika Mashariki, lakini pia niseme kuwa siyo vyuo vingi hapa duniani vimeweza kupata bahati ya kukua kwa kasi kubwa ndani ya miaka minne kama Udom, kwa hiyo ukuaji wa chuo hiki lazima uwe wa kisasa na unaokwenda na sayansi na teknolijia,” alisema
Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa Udom, Prof Idris Kikula, alisema chuo kilikuwa kinakabiliwa na tatizo katika ufundishaji, hatua iliyoulazimisha uongozi kubuni mkakati huo.Kikula alisema hatua ya sasa ni ya kuwajengea uwezo wahadhiri, ili waweze kufanyakazi zao kwa ufanisi mkubwa zaidi.


Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. KILWA FORUMS - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website
Proudly powered by Blogger